Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2020

Mambo Muhimu Kama Unataka Kufanikiwa Biashara Mtandaoni.

Mambo Muhimu Kama Unataka Kufanikiwa Biashara Mtandaoni Imeandikwa na Stepado Pascal                 Kama wewe ni mmoja wa watu ambao wanafikiria kuanza biashara yoyote mtandaoni basi nakukaribisha kwenye makala hii, Kupitia makala hii nitakwambia mambo ambayo unatakiwa kujua kabla ya kuanza biashara hiyo ikiwa pamoja na njia za muhimu za kufuata ili kufanikiwa. Kabla ya yote ni vyema niwe mkweli, mimi binafsi yangu bado sijafanikiwa kwa asilimia 100, ila pia siwezi kusema kuwa sijawahi kuona mafanikio ya biashara mtandaoni, hivyo nadhani kwa ujuzi wangu huo mdogo ninaweza kukupa mambo mawili matatu ambayo yamenisaidia mimi kuwa na mafanikio hayo madogo. Basi baada ya kusema hayo, moja kwa moja twende kwenye makala hii ya leo. Subira ni Muhimu Sana Kama wewe ulishawahi kufanya biashara yoyote basi lazima unajua kuwa biashara yoyote inahitaji subira. Hii ni muhimu sana kuliko mambo yote kwani unaweza kuwa na furaha wakat...

Je....! Kuwa na Subscriber Wengi Ndio Kupata Pesa Nyingi YouTube Au sivyo..?

Je Kuwa na Subscriber Wengi Ndio Kupata Pesa Nyingi YouTube Written by Stepado Pascal 3-4 minutes Kama wewe ni mmoja wa watu ambao wana miliki akaunti kwenye mtandao wa youtube basi pengine hii ni sababu ya wewe kusoma makala hii, kama huna akaunti kwenye mtandao wa youtube na ulikuwa unafikiria kuwa na akaunti basi pengine ni vizuri kusoma makala hii kabla ya kuendelea kwenye hatua ya kufungua channel yako. Kupitia makala hii nitaenda kukwambia ni njia gani za kutumia kupata pesa zaidi kwenye mtandao wa youtube ikiwa pamoja na kujibu baadhi ya maswali ambayo pengine yalikua yanakusumbua sana. Kwa kuanza labda tukubaliane kwamba, Subscriber ni sehemu muhimu sana  kwenye channel yako hasa kama unatarajia kuanza au ndio kwanza umeanza. Pia ukumbuke kuwa subscriber ndio kitu cha muhimu kinacho saidi wewe kuanza kutengeneza pesa kwenye channel yako kutokana na sheria ya youtube ambayo ina ainisha kuwa na subscriber pamoja na views kuanza kutengeneza pesa kupitia mtand...

Jinsi ya Kutumia Mtandao wa TikTok Hatua kwa Hatua

Jinsi ya Kutumia Mtandao wa TikTok Hatua kwa Hatua Written Stepado Pascal Mtandao wa TikTok ni moja kati ya mitandao ambayo hadi sasa imekuwa na umaarufu mkubwa sana kutokana na kutumiwa na watu mbalimbali duniani kote. Hivi karibuni inasemekana mtandao huo umekuwa kwa kasi na kuwa na watumiaji zaidi ya bilioni 1 kwa kipindi cha muda mfupi sana. Kutokana na kuwa mtandao huo umekuwa ni maarufu na kutumiwa na watu wengi sana, leo nimeona nikuandalie makala fupi na rahisi ambayo itakusaidia kujua jinsi ya kutumia mtandao wa TikTok pamoja na kufahamu kazi ya vitu mbalimbali ndani ya app hiyo. Basi bila kuendelea kupoteza muda wako zaidi twende moja kwa moja kwenye makala hii. Muonekano wa Mtandao wa TikTok Mara baada ya kupakua app ya TikTok, utaweza kupata muonekano ambao ni mrahisi kwa watumiaji wa muda mrefu, lakini kama wewe ni mgeni na hii ndio mara yako ya kwanza kutumia mtandao wa TikTok basi hivi ndivyo mtandao huo unavyo onekana kwenye ukurasa wa mwanzo. Kama u...

Tofauti ya Processor za Mediatek Helio na Qualcomm Snapdragon

Tofauti ya Processor za Mediatek Helio na Qualcomm Snapdragon Written by Stepado Pascal Kama wewe ni mmoja wa watu ambao wanatumia smartphone au umekuwa msomaji watu hapa Stepado.blogspot.com basi lazima umesha sikia tukisema sana kuhusu processor za Mediatek na Snapdragon. Sasa kutokana na mijadala mbalimbali mitandaoni kuhusu processor hizi mbili leo nimeona nikuletee makala fupi yenye kuonyesha tofauti kati ya processor za Mediatek na Snapdragon. Kupitia makala hii sitoingia ndani sana na kuanza kuzungumza historia ya kampuni hizi mbili bali nitatumia muda huu kukwambia vitu vya muhimu ambavyo nadhani vinaweza kufanya uweze kuona tofauti kati ya processor hizo mbili. Basi bila kupoteza muda twende tukangalie tofauti hizi. Utengenezaji Kwa kuanza labda tuongelee tofauti ya utengenezaji wa processor za   Mediatek Helio   na   Qualcomm Snapdragon . Kwa upande huu kampuni zote mbili hazitengenezi processor zake zenyewe bali kampuni hizi mbili zote hufanya...