Skip to main content

Je....! Kuwa na Subscriber Wengi Ndio Kupata Pesa Nyingi YouTube Au sivyo..?


Je Kuwa na Subscriber Wengi Ndio Kupata Pesa Nyingi YouTube

Written by Stepado Pascal
3-4 minutes

Kama wewe ni mmoja wa watu ambao wana miliki akaunti kwenye mtandao wa youtube basi pengine hii ni sababu ya wewe kusoma makala hii, kama huna akaunti kwenye mtandao wa youtube na ulikuwa unafikiria kuwa na akaunti basi pengine ni vizuri kusoma makala hii kabla ya kuendelea kwenye hatua ya kufungua channel yako.
Kupitia makala hii nitaenda kukwambia ni njia gani za kutumia kupata pesa zaidi kwenye mtandao wa youtube ikiwa pamoja na kujibu baadhi ya maswali ambayo pengine yalikua yanakusumbua sana.
Kwa kuanza labda tukubaliane kwamba, Subscriber ni sehemu muhimu sana kwenye channel yako hasa kama unatarajia kuanza au ndio kwanza umeanza. Pia ukumbuke kuwa subscriber ndio kitu cha muhimu kinacho saidi wewe kuanza kutengeneza pesa kwenye channel yako kutokana na sheria ya youtube ambayo ina ainisha kuwa na subscriber pamoja na views kuanza kutengeneza pesa kupitia mtandao wa YouTube.
Kama unavyoweza kuona, kwa mujibu wa youtube unahitaji kuwa na subscriber wasio pungua 1000 na views 4000 ndani ya kipindi cha mwaka mmoja au miezi 12. Hii tu ni sehemu ambayo inaonyesha kuwa subscribers ni muhimu sana tena zaidi kama unataka kuanza. Hivyo basi, wakati unafikiria kuanzisha channel kwaajili ya kujipatia kipato mtandaoni ni muhimu kuangalia subscriber ili kufikia malengo yako mapema.
Je Subscribers Wengi Ndio Pesa Nyingi Youtube.?
Jibu la moja kwa moja kwenye swali hilo ni HAPANA, kuwa na subscriber wengi haku maanishi kuwa channel fulani inaingiza kipata kwa wingi au lah. Bali hii ufikiriwa hivyo kwani watu wengi hudhania kuwa na subscriber wengi ndio hufanya watu wengi zaidi kuangalia video hivyo mtu kutengeneza kipato zaidi.
Je Kitu Gani Kinaweza Kusaidia Kutengeneza Pesa Zaidi YouTube.?
Jibu la moja kwa moja la swali hili ni VIEWS, haijalishi una subscribers wangapi kwenye channel yako kitu cha muhimu ni views. Watu wengi wanapo angalia video zako hii ina maanisha kuwa watu wengi wanaona matangazo yanayopita kwenye video zako hivyo kutengeneza pesa zaidi, hii ni muhimu kwani mtu anaweza kuona video zako bila hata kuwa mmoja wa subscribers wako. Hivyo ni muhimu kutengeneza Views nyingi zaidi kama unataka kutengeneza pesa zaidi.
Je Unawezaje Kujua Kama Channel Inatengeneza Pesa Zaidi.?
Kama unataka kujua kama channel inatengeneza pesa nyingi zaidi basi unaweza kuangalia jumla ya views ambayo inapatikana kwenye ukurasa wa about kwenye channel yako au ya mtu yoyote.
kama inavyo onekana hapa views wa channeli ya youtube

Kama unavyoweza kuona hiyo ni idadi ya views, views hizo ndio zinaweza kuonyesha kiasi cha pesa ambacho channel inaweza kutengeneza, unaweza kurekodi kwa wiki views zilikuwa ngapi alafu baada ya wiki unaweza kuangalia kujua kama views zimebadilika kwa kiasi kikubwa. Kama kuna mabadiliko makubwa basi channel hiyo inatengeneza pesa nyingi zaidi.
Je Unafanyaje Kuongeza Views Zaidi.?
Ukweli ni kwamba hata mpaka sasa binafsi najifunza kuongeza view kwenye video zetu, lakini kifupi ni kuwa hakuna njia moja ya kuongeza view kwenye video, zipo njia nyingi sana za kuongeza view ikiwa pamoja na kushare video kwenye mitandao ya kijamii na mengine mengi ya muhimu. Unaweza kufanya mambo haya machache ili kuongeza views.
ü  Andika vichwa vya habari vinavyo vutia watu zaidi.
ü  Weka Thumbnail au picha za video zinazo vutia zaidi.
ü  Tengeneza video zenye ubora.
ü  Tengeneza video zenye kutoa elimu ambayo itasaidia video zako kuangaiwa zaidi.
ü  Tengeneza video zinazodumu YouTube.
ü  Shiriki video kwenye mitandao yako ya kijamii.
ü  Tumia sehemu ya Discussion kutangaza video zako.
Mpaka hapo natumaini umejua kuwa views ni muhimu kuliko subscriber kwenye channel yako. Kumbuka ni muhimu kuweka video mpya mara kwa mara kwani hii itasaidia watu kuweza kujua channel yako na kutazamwa zaidi na hivyo kutengeneza pesa Zaidi,pia ni muhimu kuweka time table ya jinsi unavo post video katika channel yako kwani itakusaidia kuwa na watu wengi Zaidi.

stepado.blogspot.com tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi wakati wote. Nawapenda sana

Comments

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kusoma Meseji za WhatsApp Bila Kuonekana Online

  Jinsi ya Kusoma Meseji za WhatsApp Bila Kuonekana Online Written by Stepado Pascal Ni wazi kuwa katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia kuna sababu nyingi sana ambazo zinaweza kukufanya uwe na uhitaji wa kusoma meseji uliyotumiwa kupitia programu ya WhatsApp bila programu hiyo kuonyesha kama upo “online” au bila kuonyesha kama umesoma meseji hiyo. Kupitia makala hii nitaenda kuonyesha njia mpya na rahisi ambayo unaweza kutumia ili kujibu meseji zako za WhatsApp unazotumiwa bila programu ya WhatsApp kuonyesha kama upo online au bila kuonyesha kama umesoma meseji hiyo yaani tiki mbili za blue. Najua kila mtu anaweza kusema najua hiyo lakini nakushauri endelea kusoma makala hii hadi mwisho kwani unaweza kupata maujanja mapya ambayo pengine ulikuwa hujui kwa namna moja ama nyingine. Kama kawaida sipendi kupoteza muda wako mwingi kwa maneno yangu, basi bila kupoteza muda twende tukangalie njia ya kwanza. Njia ya Kwanza Najua kuwa unaweza kusema kuwa unaweza k...

Download Programu ya Microsoft Office 2019 Pro Plus

Download Programu ya Microsoft Office 2019 Pro Plus Written by STepado pascal Ikiwa tunazungumzia programu bora kwaajili ya ofisi ni wazi kuwa programu ya Microsoft Office ni programu bora sana kwako, programu hii inakuja na uwezo mkubwa sana wa kusaidia mtu ambaye anafanya kazi kwenye ofisi, au hata kama wewe ni mwanafunzi programu hii ni bora sana kwako. Kuliona hili leo nimekuletea makala ambayo itakusaidia sana kuweza kupata programu ya Microsoft Office 2019 Pro Plus, ambayo imesheheni sifa nyingi sana bure bila kulipia gharama yoyote. Kumbuka hili ni toleo la Pro Plus hivyo limesheheni sifa zote za programu ya Microsoft Office. Baadhi ya programu ambazo zipo ndani ya toleo hili ni pamoja na –     Microsoft Word     Microsoft Excel     Microsoft Powerpoint     Microsoft Outlook     OneNote     OneDrive     Microsoft Teams Kwa kuanza ni vyema kufahamu kuwa programu hii ni kwa ajili ya kompyuta za Windows na inafany...

Kuanzia A-Z List zote za Windows CMD Commands

A-Z List 0f Windows CMD Commands  By  Am IT guy STEPADO Zifuatazo ndizo   list zote za Windows CMD commands  ambazo nimezipangilia katika alphabetically CMD commands. Command Prompt  and  CMD Commands  are unknown territories for most of the Windows users, they only know it as a black screen for troubleshooting the system with some fancy commands. repair a corrupted disk, hide certain drives, to create a hacking-like environment, etc. Nini maana ya Command Prompt na CMD Commands? Command Prompt, kwa jina jingine ni  cmd.exe  or  cmd  —   ni  command line amabyo inatumika kutafsiri application  katikaWindows NT family operating systems. Na CMD Commands ni specific set of instructions given to Command Prompt to perform some kind of task or function on your Windows PC. Most of the Windows CMD Commands are used to automate tasks via script  and batch files, perform advanced administrative functi...

Jinsi ya Ku-install Windows 10, 8, 7 na XP Kwenye Simu za Android

 Jinsi ya Ku-install Windows 10, 8, 7 na XP Kwenye Simu za Android Written by STepado Pascal windows kwenye android (1) Kutokana na teknolojia kubadilika sana vile vile hata simu zetu nazo zimekua zikibadilika kila siku, simu zetu zimekuwa zimebadilika kuanzia uwezo, vitu inavyofanya mpaka matumizi ya simu hizo. kuelewa mabadiliko hayo leo Tanzania Tech tunaenda kukuonyesha njia rahisi ya kuinstall Windows 7, Windows 8, Windows 10 pamoja na Windows XP kwenye simu yako ya Android. Kwa kuanza ni vyema ukajua kuwa uwezo wa kutumia Windows kwenye simu yako unaweza kukusaidia wewe kutumia simu yako kama kompyuta, njia hii itakusaidia sana kama simu yako inauwezo wa kutumika kwenye screen kubwa ili kukupa uwezo wa kufanya vitu mbalimbali kama unavyo tumia kwenye kompyuta, yaani bila tofauti kubwa utafauti ni kwenye graphics pekee. Kwa kuanza unatakiwa kuwa na simu yako ya Android yenye RAM at-list GB 1 na kuendelea, uharaka wa kuinstall Windows kwenye simu yako unategemeana sana na Uwezo...

Njia za Kutoa Simu Yako kwenye Hali ya Kustaki (Njia Rahisi)

Njia za Kutoa Simu Yako kwenye Hali ya Kustaki (Njia Rahisi) Written by Stepado Pascal Kama wewe ni mmoja wa watu ambao wanakuwa na tatizo la simu yako kustaki mara kwa mara basi makala hii ni kwa ajili yako. Kama unavyojua, simu nyingi za Android za sasa zinakuja zikiwa zimefungwa moja kwa moja na hauwezi kufunguka simu hiyo kwa namna yoyote. Ni kweli kwamba njia rahisi ya kuweza kuondoa simu kwenye hali ya kustaki ni kutoa battery ya simu hiyo na kurudisha, lakini unafanyaje kama simu yako imefungwa moja kwa moja na huwezi kufungua simu hiyo ili kutoa battery...? Majibu ninayo. Kwanza awali ya yote labda nikwambie kuwa, hatizo hili limenikuta binafsi na katika hali ya kufanya ufumbuzi nikaona sio mbaya nikishiriki na wewe njia ambazo nilitumia kuweza kuondoa simu yangu kwenye hali ya kustaki. Kumbuka njia hizi mara nyingi zinafanya kazi kwenye simu za aina zote yaani simu za Android pamoja na simu za iPhone au iOS.Zipo njia nyingi sana lakin katika zote...

Link ya kupata windows

Mambo vp Wana blog ,leo nimekuletea link hii hapa chini ,uweze kupakuwa window yoyote uitakayo kwa matumizi yako ,hvo basi bila kupoteza wakati click hiyo link hapo itakupeleka kupakuwa windows. Ukipata changamoto yoyote niachie comments yako hapo chini au chochote Cha kushare nasi karibu Sana.Tukutane tena wakati mwingine Click hapa

Antivirus ipi Bora zaidi kwa Windows 10?

Welcome in Technology   MAADA LEO *Anti-virus Ipi ni Bora zaidi kwa Windows 10?*  *By Am IT guy STEPADO* Windows 10 haitaingilia kazi mara kwa mara kukutaarifu kupakia ‘Anti-virus’ kwenye mashine yako kama vile Windows 7 ilivyokuwa ikifanya. Hii ni kwa sababu kuanzia Windows 8, Microsoft walifanya uamuzi wa msingi wa kuweka Anti-virus moja-kwa-moja kwenye mfumo wao. Antivirus hii inaitwa Windows Defender na ni Antivirus ambayo Microsoft wenyewe wanaitoa bure pamoja na WIndows mpya. Kwa maana hiyo swali la msingi la makala hii linafaa kubadilika na kuwa – ‘Je Windows Defender ni antivurus ni bora zaidi kwa usalama wa kompyuta yako au la?’ Windows Defender WIndows Defender inatokana na Microsoft Security Essentials (MSE) na ni, kwa maneno mengine, toleo la kisasa zaidi la MSE, ambayo ilikuwa ni antivirus ya bure kabisa kwa ajili ya Windows 7. Kwa sasa, antivirus ya Windows Defender inakuja pamoja na Windows na ni ngome ya kwanza kwa kompyuta yako. *Je, Windows Defender Inatosha...