Skip to main content

Laptop 10 Bora za Kununua kwa Sasa (2020)

 

Hizi Hapa Laptop 10 Bora za Kununua kwa Sasa (2020)

Written by Stepado Pascal


Ni mda mrefu sana umepita toka tuongelee kuhusu laptop, pengine hii ni kutokana na uwepo wa laptop mpya chache sana kwenye miaka ya karibuni au ni kwa sababu simu zimekuwa zikishika chati zaidi kwa sasa pengine kuliko laptop, Lakini kama ulikua mmoja wa watu ambao wanatamani kujua kuhusu laptop bora mwaka huu (2020) kabla haujaisha maana sasa tupo jully na wewe ni kiu yako kumiliki laptop basi hii hapa ndio list ya laptop bora ambazo unaweza kununua kwa sasa.

Kumbuka laptop hizi nyingi zinapatikana hapa Tanzania hivyo tutajitahidi kuweka na bei za laptop hizi ili uweze kujua angalau kwa makadirio ni kiasi gani cha fedha unachotakiwa kuwa nacho ili uweze kupata aina flani ya laptop. Basi bila kupoteza muda twende tuka angalie list hii, Kumbuka list hii haijapangwa kwa namba hivyo laptop zote hapa ni bora sana kuwa nazo.


MacBook Pro Yenye Touch Bar

Ni wazi kuwa Macbook Pro yenye Touch Bar ni laptop bora sana ya kununua kwa sasa, kama wewe ni mmoja ya watu ambao wanafanya kazi za Ubunifu wa michoro mbalimbali (Graphics Design) basi hii ni laptop muhimu na nzuri sana kwako. Bei ya Laptop Hii ni kuanzia Milioni Tsh 3,500,000 mpaka milioni Tsh 4,000,000.

Sifa za MacBook Pro Yenye Touch Bar

  • CPU: Dual-core Intel Core i5 – i7
  • Graphics: Intel Iris Plus Graphics 640 – 650
  • RAM: 8GB – 16GB
  • Screen: 13.3-inch, (2,560 x 1,600) IPS
  • Storage: 256GB – 1TB PCIe 3.0 SSD

Mazuri Kuhusu Laptop Hii

  • Hii ndio Laptop bora kwa sasa kutoka Apple
  • Processory ya Laptop hii inafanya kazi Haraka

Mabaya Kuhusu Laptop Hii

  • Chaji yake Haidumu Sana
  • Ni Bei Ghali Sana


Microsoft Surface Book 2 (13.5-inch)

Kama wewe ni mmoja ya watu ambao wanapenda laptop inayoweza kubadilika na kuwa Tablet basi laptop hii ya Microsoft Surface Book 2 (yenye inch 13.5) ni chaguo zuri sana kwako. Mbali na uwezo wa laptop hii kuwa Tablet, laptop hii inauwezo mkubwa sana na ni nzuri sana kwa wafanyakazi wa maofisini pamoja na wanafunzi. Bei ya Laptop hii inaanzia Tsh Milioni 2,500,000 mpaka Tsh Milioni 3,500,000.

Sifa za Microsoft Surface Book 2 (13.5-inch)

  • CPU: Intel Core i5-7300U – Intel Core i7-8650U 1.9GHz
  • Graphics: Intel UHD Graphics 620; Nvidia GeForce GTX 1050 (2GB GDDR5 VRAM)
  • RAM: 8GB – 16GB
  • Screen: 3,000 x 2,000 (267 ppi) PixelSense display, 3:2 aspect ratio
  • Storage: 256GB – 1TB SSD

Kizuri Kuhusu Laptop Hii

  • Battery Yake Inadumu na Chaji
  • Laptop Hii ina nguvu Sana

Kibaya Kuhusu Laptop Hii

  • Bei Ghali
  • Haiji na Kalamu


Acer Switch 3

Kama wewe ni mpenzi wa laptop zenye uwezo wa kubadilika na kuwa Tablet basi ni vyema ufahamu laptop hii, Laptop hii ni moja kati ya laptop yenye nguvu zaidi na kizuri zaidi ni kuwa laptop hii inapatikana kwa bei rahisi. Bei ya Laptop hii inaanzia Tsh 1,000,000 hadi Tsh 1,500,000.

Sifa za Acer Switch 3

  • CPU: 1.10GHz Intel Pentium Quad Core N4200 – Intel Core i3 7100U
  • Graphics: Intel HD Graphics 505
  • RAM: 4GB
  • Screen: 12.2-inch, 1920 x 1200 IPS LCD touchscreen
  • Storage: 64GB – 128GB eMMC

Kizuri Kuhusu Laptop Hii

  • Kwa Sura ni Nzuri Sanaa
  • Bei Yake ni Rahisi

Kibaya Kuhusu Laptop Hii

  • Sio Nzuri kwa Game


Apple MacBook 12-inch (2017)

Kama wewe ni mwanafunzi au mfanyakazi ambaye unafanya kazi zako kwa kusafiri kila mara basi  Apple MacBook 12-inch (2017) ni laptop bora sana kwako, Mbali ya laptop hii kuwa na uwezo mkubwa sana pamoja na kuwa nyepesi kuibeba, vilevile laptop hii ina uwezo mkubwa sana wa kudumu na chaji hivyo inakupa uwezo wa kuendelea kufanya shughuli zako za kila siku bila kuwa na wasi wasi wa kuisha chaji kwa haraka. Bei ya laptop hii inaanzia Tsh 3,000,000 hadi Tsh 2,500,000

Sifa za Apple MacBook 12-inch (2017)

  • CPU: Intel Core M3 1.2GHz – Intel Core i7 1.4GHz
  • Graphics: Intel HD Graphics 615
  • RAM: 8GB – 16GB
  • Screen: 12-inch, (2,304 x 1,440) IPS 16:10
  • Storage: 256GB – 512GB SSD

Kizuri Kuhusu Laptop Hii

  • Processor Yenye Nguvu Zaidi
  • Battery Inadumu na Chaji Zaidi

Kibaya Kuhusu Laptop Hii

  • Inayo Sehemu Moja ya USB-C port
  • Ni Bei Ghali


Lenovo Yoga 920

Laptop hii pia ni moja kati ya laptop zenye uwezo wa kubadilika na kuwa tablet, lakini utofauti wa laptop hii ni kuwa, Laptop hii haitoki kama zilivyo laptop nyingine kwenye list hii, Laptop hii yenyewe inazunguka nyuzi 360 na kukupa uwezo wa kufanya laptop hiyo kuwa tablet. Kama wewe ni mwanafunzi au mfanyakazi wa ofisini laptop hii itakufaa sana. Bei ya laptop hii inaanzia Tsh 4,500,000 hadi Tsh 3,500,000.

Sifa za Lenovo Yoga 920

  • CPU: Intel Core i7-855OU
  • Graphics: Intel UHD Graphics 620
  • RAM: 8GB – 16GB
  • Screen: 13.9-inch 1920 x 1080 – 13.9-inch 3840 x 2160
  • Storage: 256GB – 1TB SSD
  • Connectivity: 802.11ac Wi-Fi; Bluetooth 4.1
  • Camera: 720p front-facing

Kizuri Kuhusu Laptop Hii

  • Inayo nguvu Sana ya Processor
  • Ni nyembamba

Kibaya Kuhusu Laptop Hii

  • Bei Ghali
  • Haina Uwezo Mzuri wa Graphics
  • Feni za Laptop Hii Zinatabia ya Kutoa Sauti


Asus Transformer Mini T102HA

Kama wewe unatafuta laptop ya bei rahisi yenye uwezo wa kawaida basi laptop hii ni bora sana kwako, Laptop hii ni nzuri sana kwa kufanya kazi ndogo ndogo za kila siku huku ikikupa uwezo wa kufungua kurasa mbalimbali za tovuti pamoja na kazi zingine za kawaida. Bei ya Laptop Hii ina anzia Tsh 1,000,000 mpaka Tsh 1,500,000.

Sifa za Asus Transformer Mini T102HA

  • CPU: Intel Atom x5-Z8350
  • Graphics: Intel HD Graphics – Intel HD Graphics 400
  • RAM: 2GB – 4GB
  • Screen: 11.6-inch 1,366 x 768 HD IPS touchscreen
  • Storage: 32GB

Kizuri Kuhusu Laptop Hii

  • Laptop Hii ni Ndogo kwa Umbo na Nyepesi
  • Inayo Uwezo Mkubwa wa Kudumu na Chaji

Kibaya Kuhusu Laptop Hii

  • Haina Uwezo Mkubwa Sana


Asus Zenbook UX310UA

Kama wewe ni mtu unae hitajika kufanya kazi kwa haraka kama vile mwandishi wa habari au watu walioko kwenye kazi kama hizo, basi laptop hii ni bora sana kuwa nayo. Laptop hii inasifika sana kwa tabia yake ya kuweza kuwaka kwa haraka na uwezo wake mzuri wa Processor. Bei ya Laptop Hii ina anzia Tsh 2,000,000 hadi Tsh 2,500,000.

Sifa za Asus Zenbook UX310UA

  • CPU: Intel Core i3 – i5
  • Graphics: Intel HD Graphics 620
  • RAM: 8GB
  • Screen: 13.3-inch up to QHD+ (3,200 x 1,800)
  • Storage: 256GB SSD

Kizuri Kuhusu Laptop Hii

  • Inauwezo wa Kuwaka na Kutumika Haraka

Kibaya Kuhusu Laptop Hii

  • Battery Yake Haina Uwezo wa Kudumu Sana


Dell XPS 13

Hii ni moja kati ya laptop bora sana, Kama wewe ni Mfanyakazi wa ofisi au mfanyakazi wa maswala ya ubunifu au mtengenezaji wa Video laptop hii inauwezo wa kukuhudumia Vizuri, Laptop hii ni moja kati ya laptop zenye nguvu na zinazo sifika kuwa laptop bora sana. Kama ukituuliza Tanzania Tech ni laptop gani nzuri inayo tumia Windows ambayo unaweza kununua ambayo itakusaidia hata kwa miaka ya mbeleni, basi Dell XPS 13 ni moja ya Laptop hizo ambazo tungekushauri kununua. Bei ya Laptop Hii ina anzia Tsh 5,000,000 hadi Tsh 6,000,000.

Sifa za Dell XPS 13

  • CPU: 8th generation Intel Core i5 – i7
  • Graphics: Intel UHD Graphics 620
  • RAM: 8GB – 16GB
  • Screen: 13.3-inch FHD (1,920 x 1,080) – 4k (3840 x 2160)
  • Storage: 256GB – 1TB SSD

Kizuri Kuhsu Laptop Hii

  • Inayo Uwezo wa 4K
  • Uwezo Mzuri wa Gharphics (Japo Sio Sana)

Kibaya Kuhusu Laptop Hii

  • Bei Ghali Sana


Lenovo Yoga Book

Kama wewe unatafuta laptop ya bei nafuu na yenye uwezo wa tofauti kidogo basi Laptop Hii ni moja kati ya laptop zitakazo kufaa sana. Laptop hii inauwezo mzuri sana wa kioo pamoja na uwezo wake wa kubebeka kirahisi kutokana na uzito wake mdogo. Bei ya Laptop Hii Inaanzia Tsh 800,000 hadi Tsh 1,000,000.

Sifa za Lenovo Yoga Book

  • CPU: Intel Atom x5-Z8550
  • Graphics: Intel Atom
  • RAM: 4GB
  • Screen: 10.1-inch full HD IPS touchscreen
  • Storage: 64GB SSD, up to 128GB microSD

Kizuri Kuhusu Laptop Hii

  • Laptop Hii ni Nyepesi na Nyembamba
  • Kioo Kizuri
  • Bei Rahisi

Kibaya Kuhusu Laptop Hii

  • Inatumia Processor Yenye Uwezo Mdogo


Dell XPS 15

Sasa hapa naomba niwe wazi, Laptop hii ni moja kati ya laptop ninayo ipenda sana na kuitamani sana kuwa nayo, hivyo basi inawezekana mapenzi yangu ni moja kati ya sababu ya laptop hii kuwepo hapa. Pamoja na hayo nikisema laptop bora basi hii ni moja kati ya laptop bora sana na yenye uwezo mzuri sana. Kwa mujibu wa tovuti ya Techradar Hii ndio laptop bora kutoka Dell Mpaka Sasa. Bei ya Laptop Hii ina anzia Tsh 2,500,000 hadi Tsh 3,500,000.

Sifa za Dell XPS 15

  • CPU: Intel Core i5-7300HQ – i7-7700HQ
  • Graphics: NVIDIA® GeForce GTX 1050 with 4GB GDDR5
  • RAM: 8GB – 16GB DDR4
  • Screen: Up to 15.6-inch Ultra HD (3840 x 2160) InfinityEdge touchscreen
  • Storage: 1TB HDD – 512GB SSD

Kizuri Kuhusu Laptop Hii

  • Inadumu na Chaji
  • Kioo Bora
  • Uwezo Mzuri wa Processor

Kibaya Kuhusu Laptop Hii

  • Kamera Yake (Web Cam) Imekaa Mahali Pabaya

Na hiyo ndio list ya Laptop bora ambazo unaweza kununua kwa sasa na vilevile hizi ndio laptop bora mpaka sasa mwaka huu 2019 – 2020.Tukutane tena wakati mwingine..

 

Comments

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kusoma Meseji za WhatsApp Bila Kuonekana Online

  Jinsi ya Kusoma Meseji za WhatsApp Bila Kuonekana Online Written by Stepado Pascal Ni wazi kuwa katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia kuna sababu nyingi sana ambazo zinaweza kukufanya uwe na uhitaji wa kusoma meseji uliyotumiwa kupitia programu ya WhatsApp bila programu hiyo kuonyesha kama upo “online” au bila kuonyesha kama umesoma meseji hiyo. Kupitia makala hii nitaenda kuonyesha njia mpya na rahisi ambayo unaweza kutumia ili kujibu meseji zako za WhatsApp unazotumiwa bila programu ya WhatsApp kuonyesha kama upo online au bila kuonyesha kama umesoma meseji hiyo yaani tiki mbili za blue. Najua kila mtu anaweza kusema najua hiyo lakini nakushauri endelea kusoma makala hii hadi mwisho kwani unaweza kupata maujanja mapya ambayo pengine ulikuwa hujui kwa namna moja ama nyingine. Kama kawaida sipendi kupoteza muda wako mwingi kwa maneno yangu, basi bila kupoteza muda twende tukangalie njia ya kwanza. Njia ya Kwanza Najua kuwa unaweza kusema kuwa unaweza k...

Download Programu ya Microsoft Office 2019 Pro Plus

Download Programu ya Microsoft Office 2019 Pro Plus Written by STepado pascal Ikiwa tunazungumzia programu bora kwaajili ya ofisi ni wazi kuwa programu ya Microsoft Office ni programu bora sana kwako, programu hii inakuja na uwezo mkubwa sana wa kusaidia mtu ambaye anafanya kazi kwenye ofisi, au hata kama wewe ni mwanafunzi programu hii ni bora sana kwako. Kuliona hili leo nimekuletea makala ambayo itakusaidia sana kuweza kupata programu ya Microsoft Office 2019 Pro Plus, ambayo imesheheni sifa nyingi sana bure bila kulipia gharama yoyote. Kumbuka hili ni toleo la Pro Plus hivyo limesheheni sifa zote za programu ya Microsoft Office. Baadhi ya programu ambazo zipo ndani ya toleo hili ni pamoja na –     Microsoft Word     Microsoft Excel     Microsoft Powerpoint     Microsoft Outlook     OneNote     OneDrive     Microsoft Teams Kwa kuanza ni vyema kufahamu kuwa programu hii ni kwa ajili ya kompyuta za Windows na inafany...

Kuanzia A-Z List zote za Windows CMD Commands

A-Z List 0f Windows CMD Commands  By  Am IT guy STEPADO Zifuatazo ndizo   list zote za Windows CMD commands  ambazo nimezipangilia katika alphabetically CMD commands. Command Prompt  and  CMD Commands  are unknown territories for most of the Windows users, they only know it as a black screen for troubleshooting the system with some fancy commands. repair a corrupted disk, hide certain drives, to create a hacking-like environment, etc. Nini maana ya Command Prompt na CMD Commands? Command Prompt, kwa jina jingine ni  cmd.exe  or  cmd  —   ni  command line amabyo inatumika kutafsiri application  katikaWindows NT family operating systems. Na CMD Commands ni specific set of instructions given to Command Prompt to perform some kind of task or function on your Windows PC. Most of the Windows CMD Commands are used to automate tasks via script  and batch files, perform advanced administrative functi...

Jinsi ya Ku-install Windows 10, 8, 7 na XP Kwenye Simu za Android

 Jinsi ya Ku-install Windows 10, 8, 7 na XP Kwenye Simu za Android Written by STepado Pascal windows kwenye android (1) Kutokana na teknolojia kubadilika sana vile vile hata simu zetu nazo zimekua zikibadilika kila siku, simu zetu zimekuwa zimebadilika kuanzia uwezo, vitu inavyofanya mpaka matumizi ya simu hizo. kuelewa mabadiliko hayo leo Tanzania Tech tunaenda kukuonyesha njia rahisi ya kuinstall Windows 7, Windows 8, Windows 10 pamoja na Windows XP kwenye simu yako ya Android. Kwa kuanza ni vyema ukajua kuwa uwezo wa kutumia Windows kwenye simu yako unaweza kukusaidia wewe kutumia simu yako kama kompyuta, njia hii itakusaidia sana kama simu yako inauwezo wa kutumika kwenye screen kubwa ili kukupa uwezo wa kufanya vitu mbalimbali kama unavyo tumia kwenye kompyuta, yaani bila tofauti kubwa utafauti ni kwenye graphics pekee. Kwa kuanza unatakiwa kuwa na simu yako ya Android yenye RAM at-list GB 1 na kuendelea, uharaka wa kuinstall Windows kwenye simu yako unategemeana sana na Uwezo...

Njia za Kutoa Simu Yako kwenye Hali ya Kustaki (Njia Rahisi)

Njia za Kutoa Simu Yako kwenye Hali ya Kustaki (Njia Rahisi) Written by Stepado Pascal Kama wewe ni mmoja wa watu ambao wanakuwa na tatizo la simu yako kustaki mara kwa mara basi makala hii ni kwa ajili yako. Kama unavyojua, simu nyingi za Android za sasa zinakuja zikiwa zimefungwa moja kwa moja na hauwezi kufunguka simu hiyo kwa namna yoyote. Ni kweli kwamba njia rahisi ya kuweza kuondoa simu kwenye hali ya kustaki ni kutoa battery ya simu hiyo na kurudisha, lakini unafanyaje kama simu yako imefungwa moja kwa moja na huwezi kufungua simu hiyo ili kutoa battery...? Majibu ninayo. Kwanza awali ya yote labda nikwambie kuwa, hatizo hili limenikuta binafsi na katika hali ya kufanya ufumbuzi nikaona sio mbaya nikishiriki na wewe njia ambazo nilitumia kuweza kuondoa simu yangu kwenye hali ya kustaki. Kumbuka njia hizi mara nyingi zinafanya kazi kwenye simu za aina zote yaani simu za Android pamoja na simu za iPhone au iOS.Zipo njia nyingi sana lakin katika zote...

Link ya kupata windows

Mambo vp Wana blog ,leo nimekuletea link hii hapa chini ,uweze kupakuwa window yoyote uitakayo kwa matumizi yako ,hvo basi bila kupoteza wakati click hiyo link hapo itakupeleka kupakuwa windows. Ukipata changamoto yoyote niachie comments yako hapo chini au chochote Cha kushare nasi karibu Sana.Tukutane tena wakati mwingine Click hapa

Antivirus ipi Bora zaidi kwa Windows 10?

Welcome in Technology   MAADA LEO *Anti-virus Ipi ni Bora zaidi kwa Windows 10?*  *By Am IT guy STEPADO* Windows 10 haitaingilia kazi mara kwa mara kukutaarifu kupakia ‘Anti-virus’ kwenye mashine yako kama vile Windows 7 ilivyokuwa ikifanya. Hii ni kwa sababu kuanzia Windows 8, Microsoft walifanya uamuzi wa msingi wa kuweka Anti-virus moja-kwa-moja kwenye mfumo wao. Antivirus hii inaitwa Windows Defender na ni Antivirus ambayo Microsoft wenyewe wanaitoa bure pamoja na WIndows mpya. Kwa maana hiyo swali la msingi la makala hii linafaa kubadilika na kuwa – ‘Je Windows Defender ni antivurus ni bora zaidi kwa usalama wa kompyuta yako au la?’ Windows Defender WIndows Defender inatokana na Microsoft Security Essentials (MSE) na ni, kwa maneno mengine, toleo la kisasa zaidi la MSE, ambayo ilikuwa ni antivirus ya bure kabisa kwa ajili ya Windows 7. Kwa sasa, antivirus ya Windows Defender inakuja pamoja na Windows na ni ngome ya kwanza kwa kompyuta yako. *Je, Windows Defender Inatosha...