Skip to main content

Futa Vitu Kwenye Recycle Bin Unapozima Kompyuta


Written by Stepado Pascal


Futa Vitu Kwenye Recycle Bin Unapozima Kompyuta


Kuna wakati mtu unakuwa na haraka ya kutumia kompyuta yako kiasi kwamba unasahau kufuta vitu kwenye recycle bin ya kompyuta yako, kupitia njia hii leo nitakuonyesha njia ambayo unaweza kutumia ili vitu vilivyopo kwenye recycle bin vijifute vyenyewe pale unapozima kompyuta yako.

Kabla ya kuanza labda nikueleze ni maana ya Recycle bin, kama wewe ni mtumiaji wa kompyuta kwa muda mrefu basi lazima unajua sehemu hii, kama wewe ni mgeni wa kutumia kompyuta basi ni vyema ufahamu kuwa sehemu hii ni ile ambayo ukifuta kitu kinahifadhiwa humo kwaajili ya kusubiria kufutwa kabisa au kuondolewa moja kwa moja kwenye kompyuta yako.



Sasa lengo la maujanja ya siku ya leo ni kusaidia kufuta vitu vilivyomo kwenye Recycle bin pale tu unapozima kompyuta yako, njia hii itakusaidia zaidi kama kompyuta yako ina nafasi ndogo kwani hiitasaidia kuondoa baadhi ya mafile ambayo hayana kazi au hayatumiki tena.

Pia kwa kutumia njia hii itakusaidia kama unatumia kompyuta ambayo sio ya kwako, kwani hii itakusaidia kufuta vitu vyote ambayo ulifuta wakati unatumia kompyuta hiyo ambayo pengine uliazima.

Lakini pia kama unatumia Recycle bin kama sehemu ya kuficha vitu basi njia hii haitokuwa muhimu sana kwako kwani itafanya upoteze mafile yako yote. Basi baada ya kusema hayo twende tukangalie njia hizi.

Kwa kuanza ingia kwenye Desktop yako kisha fungua application ya Notepad kisha copy na paste code hizo hapo chini kwenye ukurasa huo wa Notepad. Bofya hapo chini kucopy code hizo.

Tembelea Tovuti Hii



Baada ya hapo badilisha format ya .txt na kisha weka .bat alafu Save code hizo kwenye kompyuta yako. Baada ya hapo bofya mara mbili code hizo na utaona vitu vilivyopo kwenye Recycle bin vimefutika, kama havija futika basi angalia labda kuna kitu umekose rudia tena kwa kufuata maelezo kwa usahihi zaidi.

Hakikisa file linasomeka kwa mfano kufuta.bat na sio kufuta.txt, baada ya kufanya hatua hizo hapo juu sasa nenda kwenye sehemu ya ku-search kwenye kompyuta yako kisha andika “gpedit.msc” bila alama za funga na fungua semialafu bofya enter kwenye keyboard yako.

Baada ya hapo litafuguka jedwali lenye jina Local group policy editor, kuwa makini na sehemu hii kwani hapa ndipo panapo endesha kompyuta yako nzima. Baada ya kufungua jedwali hili, upande wa kushoto chagua Windows Settings, kisha utaona page nyingine imefunguka tena kwa chini, Tafuta sehemu iliyo andikwa Scripts (Startup/Shutdown), bofya hapo mara mbili kisha chagua Shutdown kwa kubofya mara mbili.

Baada ya hapo ukurasa mwingine utafunguka kisha bofya sehemu ya Add kwenye kibox alafu bofya Browse kisha chagua mahali ulipo hifadhi zile code zenye jina kwa mfano kufuta.bat kisha bofya Open. Baada ya hapo utakuwa umemaliza zoezi zima na sasa utakuwa upo tayari kufuta mafile yako kwenye recycle bin kila mara unapozima kompyuta yako.



Hiyo ndio njia rahisi unayoweza kutumia pale unapotaka kufuta mafile kwenye recycle bin kwa haraka Zaidi.

Kama kuna mahali umekwama au hujaelewa unaweza kuuliza kupitia sehemu ya maoni hapo chini nasi tutakujibu kwa haraka.

 

Solutions Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kusoma Meseji za WhatsApp Bila Kuonekana Online

  Jinsi ya Kusoma Meseji za WhatsApp Bila Kuonekana Online Written by Stepado Pascal Ni wazi kuwa katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia kuna sababu nyingi sana ambazo zinaweza kukufanya uwe na uhitaji wa kusoma meseji uliyotumiwa kupitia programu ya WhatsApp bila programu hiyo kuonyesha kama upo “online” au bila kuonyesha kama umesoma meseji hiyo. Kupitia makala hii nitaenda kuonyesha njia mpya na rahisi ambayo unaweza kutumia ili kujibu meseji zako za WhatsApp unazotumiwa bila programu ya WhatsApp kuonyesha kama upo online au bila kuonyesha kama umesoma meseji hiyo yaani tiki mbili za blue. Najua kila mtu anaweza kusema najua hiyo lakini nakushauri endelea kusoma makala hii hadi mwisho kwani unaweza kupata maujanja mapya ambayo pengine ulikuwa hujui kwa namna moja ama nyingine. Kama kawaida sipendi kupoteza muda wako mwingi kwa maneno yangu, basi bila kupoteza muda twende tukangalie njia ya kwanza. Njia ya Kwanza Najua kuwa unaweza kusema kuwa unaweza k...

Download Programu ya Microsoft Office 2019 Pro Plus

Download Programu ya Microsoft Office 2019 Pro Plus Written by STepado pascal Ikiwa tunazungumzia programu bora kwaajili ya ofisi ni wazi kuwa programu ya Microsoft Office ni programu bora sana kwako, programu hii inakuja na uwezo mkubwa sana wa kusaidia mtu ambaye anafanya kazi kwenye ofisi, au hata kama wewe ni mwanafunzi programu hii ni bora sana kwako. Kuliona hili leo nimekuletea makala ambayo itakusaidia sana kuweza kupata programu ya Microsoft Office 2019 Pro Plus, ambayo imesheheni sifa nyingi sana bure bila kulipia gharama yoyote. Kumbuka hili ni toleo la Pro Plus hivyo limesheheni sifa zote za programu ya Microsoft Office. Baadhi ya programu ambazo zipo ndani ya toleo hili ni pamoja na –     Microsoft Word     Microsoft Excel     Microsoft Powerpoint     Microsoft Outlook     OneNote     OneDrive     Microsoft Teams Kwa kuanza ni vyema kufahamu kuwa programu hii ni kwa ajili ya kompyuta za Windows na inafany...

Kuanzia A-Z List zote za Windows CMD Commands

A-Z List 0f Windows CMD Commands  By  Am IT guy STEPADO Zifuatazo ndizo   list zote za Windows CMD commands  ambazo nimezipangilia katika alphabetically CMD commands. Command Prompt  and  CMD Commands  are unknown territories for most of the Windows users, they only know it as a black screen for troubleshooting the system with some fancy commands. repair a corrupted disk, hide certain drives, to create a hacking-like environment, etc. Nini maana ya Command Prompt na CMD Commands? Command Prompt, kwa jina jingine ni  cmd.exe  or  cmd  —   ni  command line amabyo inatumika kutafsiri application  katikaWindows NT family operating systems. Na CMD Commands ni specific set of instructions given to Command Prompt to perform some kind of task or function on your Windows PC. Most of the Windows CMD Commands are used to automate tasks via script  and batch files, perform advanced administrative functi...

Jinsi ya Ku-install Windows 10, 8, 7 na XP Kwenye Simu za Android

 Jinsi ya Ku-install Windows 10, 8, 7 na XP Kwenye Simu za Android Written by STepado Pascal windows kwenye android (1) Kutokana na teknolojia kubadilika sana vile vile hata simu zetu nazo zimekua zikibadilika kila siku, simu zetu zimekuwa zimebadilika kuanzia uwezo, vitu inavyofanya mpaka matumizi ya simu hizo. kuelewa mabadiliko hayo leo Tanzania Tech tunaenda kukuonyesha njia rahisi ya kuinstall Windows 7, Windows 8, Windows 10 pamoja na Windows XP kwenye simu yako ya Android. Kwa kuanza ni vyema ukajua kuwa uwezo wa kutumia Windows kwenye simu yako unaweza kukusaidia wewe kutumia simu yako kama kompyuta, njia hii itakusaidia sana kama simu yako inauwezo wa kutumika kwenye screen kubwa ili kukupa uwezo wa kufanya vitu mbalimbali kama unavyo tumia kwenye kompyuta, yaani bila tofauti kubwa utafauti ni kwenye graphics pekee. Kwa kuanza unatakiwa kuwa na simu yako ya Android yenye RAM at-list GB 1 na kuendelea, uharaka wa kuinstall Windows kwenye simu yako unategemeana sana na Uwezo...

Njia za Kutoa Simu Yako kwenye Hali ya Kustaki (Njia Rahisi)

Njia za Kutoa Simu Yako kwenye Hali ya Kustaki (Njia Rahisi) Written by Stepado Pascal Kama wewe ni mmoja wa watu ambao wanakuwa na tatizo la simu yako kustaki mara kwa mara basi makala hii ni kwa ajili yako. Kama unavyojua, simu nyingi za Android za sasa zinakuja zikiwa zimefungwa moja kwa moja na hauwezi kufunguka simu hiyo kwa namna yoyote. Ni kweli kwamba njia rahisi ya kuweza kuondoa simu kwenye hali ya kustaki ni kutoa battery ya simu hiyo na kurudisha, lakini unafanyaje kama simu yako imefungwa moja kwa moja na huwezi kufungua simu hiyo ili kutoa battery...? Majibu ninayo. Kwanza awali ya yote labda nikwambie kuwa, hatizo hili limenikuta binafsi na katika hali ya kufanya ufumbuzi nikaona sio mbaya nikishiriki na wewe njia ambazo nilitumia kuweza kuondoa simu yangu kwenye hali ya kustaki. Kumbuka njia hizi mara nyingi zinafanya kazi kwenye simu za aina zote yaani simu za Android pamoja na simu za iPhone au iOS.Zipo njia nyingi sana lakin katika zote...

Link ya kupata windows

Mambo vp Wana blog ,leo nimekuletea link hii hapa chini ,uweze kupakuwa window yoyote uitakayo kwa matumizi yako ,hvo basi bila kupoteza wakati click hiyo link hapo itakupeleka kupakuwa windows. Ukipata changamoto yoyote niachie comments yako hapo chini au chochote Cha kushare nasi karibu Sana.Tukutane tena wakati mwingine Click hapa

Antivirus ipi Bora zaidi kwa Windows 10?

Welcome in Technology   MAADA LEO *Anti-virus Ipi ni Bora zaidi kwa Windows 10?*  *By Am IT guy STEPADO* Windows 10 haitaingilia kazi mara kwa mara kukutaarifu kupakia ‘Anti-virus’ kwenye mashine yako kama vile Windows 7 ilivyokuwa ikifanya. Hii ni kwa sababu kuanzia Windows 8, Microsoft walifanya uamuzi wa msingi wa kuweka Anti-virus moja-kwa-moja kwenye mfumo wao. Antivirus hii inaitwa Windows Defender na ni Antivirus ambayo Microsoft wenyewe wanaitoa bure pamoja na WIndows mpya. Kwa maana hiyo swali la msingi la makala hii linafaa kubadilika na kuwa – ‘Je Windows Defender ni antivurus ni bora zaidi kwa usalama wa kompyuta yako au la?’ Windows Defender WIndows Defender inatokana na Microsoft Security Essentials (MSE) na ni, kwa maneno mengine, toleo la kisasa zaidi la MSE, ambayo ilikuwa ni antivirus ya bure kabisa kwa ajili ya Windows 7. Kwa sasa, antivirus ya Windows Defender inakuja pamoja na Windows na ni ngome ya kwanza kwa kompyuta yako. *Je, Windows Defender Inatosha...